Inj.Hussen Nyemba ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Makambako (MAKUWASA) aliyeteuliwa na ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mnamo Septemba 1, 2016
Kabla ya uteuzi Inj.Hussen Nyemba alikuwa akifanyakazi Halmashauri ya Mji Makambako kama Muhandisi wa Maji katika Idara ya Maji mnamo Novemba 17,2014 hadi Agosti 30,2016.
Pia amefanya kazi katika Halmashauri ya Wilaya na Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Ludewa kama fundi sanifu na badae kama Mhandisi wa Maji baada ya kupata shahada ya kwanza ya uhandisi wa ujenzi na rasilimali maji katika chuo kikuu cha Ardhi kilichopo jijini Dar es salaam.
Inj.Hussen Nyemba amezaliwa tarehe 15.03.1988 katika wilaya ya Ilala mkoa wa Dar es salaam , Nakusoma diploma ya Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira katika chuo cha Maji kilichopo Ubungo jijijni Dar es salaam mnamo mwaka 2006 na kuhitimu mwaka 2009 na kuajiriwa kama fundi sanifu upandewa maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa. Mwaka 2010 Inj.Hussen Nyemba alijiunga na chuo cha Ardhi Dar es salaam kusomea shahada ya ujenzi na Rasilimali Maji na kuhitimu mwaka 2014.
Inj. Hussein Nyemba tangu ateuliwe kuwa mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Makambako kwa kushirikiana na Bodi ya Maji, watumishi wa MAKUWASA pamoja na wadau mbalimbali amefanikiwa mambo katika kuhakikisha Mamlaka ya Maji Makambako inasonga mbele katika kutoa huduma bora ya maji kwa wananchi wa Makambako.
.
Makambako
Anuani ya posta: P.O.Box 940 Makambako
Simu: +255 262730407
Simu ya kiganjani: 08000750041
Baruapepe za Watumishi: md@makuwa.go.tz
Copyright ©2018 Makuwasa . All rights reserved.